"Uhuru ni Jasho"
Tumuunge mkono Mhe Rais @MagufuliJP kwa kufanya usafi tukiadhimisha siku ya Uhuru wetu. pic.twitter.com/XgoNPt3kyx
— Chama Cha Mapinduzi (@ccm_tanzania) December 9, 2015
Dotto
Kahindi
Leo Tanzania
inaazimisha miaka 54 ya Uhuru wake. Katika karne hii ya sayansi na teknolojia
Uhuru wa mtu, jamii, nchi ama taifa unapaswa kuendana na Maendeleo. Bila kuwepo
maendeleo ni vigumu kufanikiwa kwa uhuru huo kikamilifu.
Happy Uhuru Day #Tanganyika #ProudlyTanganyikan hata kama wengine wanajisahaulisha makusudi na kusema "Uhuru wa TZ" pic.twitter.com/MvA2osPtX5
— Naamala (@NaamalaSamson) December 9, 2015
Katika
kitabu chake Mwl Nyerere cha Uhuru na Maendeleo, anasema kuwa Uhuru na Maendeleleo
ni vitu vinavohusiana sana. Uhusiano wake ni kama kuku na yai, bila ya kuku
hupati yai, na bila ya mayai hupati kuku, vivyo hivyo bila ya uhuru hupati
maendeleo na bila ya maendeleo uhuru hautakuwepo.
Hata hivyo
maendeleo ya nchi yanahitaji usafi, si usafi wa kuchukua fagio na nyenzo nyingine
za kufanyia usafi ili kusafisha, kuzibua na kutindua makoko ya uchafu ambayo
yamekwama katika maeneo yetu bali ni usafi wa mioyo yetu pia
Kwa kuona
umuhimu wa usafi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli akaamua kuwa maadhimisho ya Sherehe za Uhuru na Jamhuri tarehe 9
Desemba, 2015, yatumike kwa kufanya kazi na usafi
Rais Magufuli hapa uko sawa
kabisa, hujakosea maana Watanzani tumejawa na roho chafu, uzembe, mifereji na
mitaro ya fikra zetu imeziba, na inahitaji kuzibulia ili tuweze kufikiria
sawasawa.
Mitaro ya ufisadi, rushwa,
magonjwa, kukosa uwajibikaji, elimu duni, umasikini, ujinga vinahitaji siku
maalumu kuviondoa, na siku hii ni 9 desemba, siku ya uhuru, tunataka tuwe huru
kwelikweli.
Ni vizuri kuitumia siku hii
kutafakari na kuziondoa taka ndani ya moyo wako, nafsi yako, taka kwenye mwili
wako, kazini kwako, nyumbani kwako, na zile taka ngumu za kukosa uzalendo ili
sote tuifurahie Tanzania iliyosafi na salama pasi na kipindupindu.