MKAA POA NI UTATUZI WA UHARIBIFU WA MAZINGIRA – MPINA

  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina  akizungumza katika eneo la uzalishaji mkaa, katika kiwand... thumbnail 1 summary
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akizungumza katika eneo la uzalishaji mkaa, katika kiwanda cha mkaa poa, mkaa rafiki kwa mazingira mjini Unguja, Kulia ni mmoja wa wafanyakazi katika kiwanda hicho kidogo.
Sample ya Mkaa Poa ulioanikwa juani tayari kupakiwa na kuuuzwa kwa matumizi ya nyumbani
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akiangalia mkaa unaoendelea kuwaka moto katika jiko la mkaa ambapo mkaa huo unadaiwa kuwaka kwa masaa matatu.
 Mkurugenzi wa Kiwanda cha Mkaa Poa cha Mjini Unguja Bw. Bukhet Juma Pamoja na Naibu Waziri Mpina wakiangalia mkaa uliyopo tayari kwamatumizi ya nyumbani.
 Wafanyakazi wa kiwanda kidogo chakutengeza mkaa banifu, mkaa rafiki kwa mazingira maarufu kwa jina la Mkaa poa Mjini Unguja wakiwa katika Picha ya Pamoja na Naibu Waziri Mpina Kiwandani hapo.
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akiongea na uongozi wa Mradi wa muungano wa MIVARF pamoja na ujumbe wake katika ziara Mjini Unguja ilohusisha kutembelea Miradi ya Muungano.
Sehemu la eneo la Mto lilitengenezwa na Mradi wa MIVARF katika Mkoa wa Kusini Unguja ili kuweza kusaidia wakaazi wa maeneo ya mabondeni kufanya kilimo hasa katika kipindi cha mvua.



NA Evelyn Mkokoi - Unguja
Jamii inaweza kuhepukana na mgogoro wa uchafuzi na uharibifu wa mazingira, utakanao na kukata miti ovyo kwa matumizi ya mkaa, kama itakuwa na ubunifu wa kutumia teknolojia ya kisasa ya kutengeneza mkaa banifu aina ya mkaa Poa ambayo ni rafiki wa mazingira,
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais anaeshungulikia Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, ameyasema hayo leo Mjini Unguja alipotembelea kiwanda cha kutengeza mkaa banifu maarufu kama mkaa poa.
Mpina alisema kuwa ukataji ovyo wa miti ya mikoko katika jamii ya pwani kwa matumizi ya mkaa ni changamoto kubwa ambapo jamii hizi za pwani zikibuni na kuiga teknolojia ya kutengeneza mkaa kwa kutumia mali ghafi za taka za mbao yani maranda, taka za maganda ya miwa na taka nyingine laini, zitakuwa zimejibu tatizo la ukataji wa miti kwa matumizi ya mkaa.
“Matumizi endelevu ya malighafi za taka na mabaki mengine yanaweza kuwaletea wanachi faida zaidi hasa wakiingia katika biashara hii ya mkaa poa na kunusuru mazingira, hivyo natoa wito kwa wamiliki wa kiwanda hiki cha mkaa, waendelee kupanua uzalishaji na kuongeza soko la bidhaa hii hata kwa upande mwigine wa muungano ili asilimia kubwa ya watanzania ijifunze kutunza mazingira kwani mkaa huu ni wa bei nafuu, Na wapanue teknolojia hii na kunusuru mazingira ”Alisisitiza Mpina.
Aidha, Mpina aliishauri serikali kuendela kuunga mkono jitihada za kampuni hiyo inayotengeza mkaa poa, na watanzania wengine wenye kufanya biashara za mkaa banifu, ili kuhepusha uharibifu wamazingira, kunusuru nchi kuwa jangwa na kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi.

Akiwa Mjini Unguja Naibu Waziri Mpina pia alitembelea miradi ya muungano iliyopo chini ya TASAF na MIVARF  na kuwapongeza waratibu wa miradi hiyo kwa kuisimamia vizuri na kujitahidi kwa kiasi Fulani kutatua matatizo na wananchi na kuwaasa kuchukua taadhari katika utekelezaji wa miradi yao ili kuweza kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi hususan katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji hasa katika kipindi hiki ambacho msimu wa mvua umekuwa ukibadilika mara kwa mara.